Skip to main content

Zari Yamfika Mazito Kutoka Kwa Wananzengo

Mwanamama mjasiriamali, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ ambaye ni mzazi mwenza wa staa wa muziki barani afrika, Nasibu abdul ‘Diamond Platnumz’ yamemfika mazito kutoka kwa wananzengo, kisa kikiwa ni mwanamitindo maarufu Bongo, Hamisa Mobeto.

Chanzo cha yote ni baada ya Mobeto kumposti Diamond au Mondi ambaye naye pia ni mzazi mwenzake kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Zari amejikuta akishambuliwa kutokana na kile alichokiposti Mobeto kuhusu Mondi kuwepo nyumbani kwake huku akiwa na mtoto wao, Abdul Nasibu ‘Dyllan’.

Mobeto aliposti video kwenye ukurasa wake wa Instagram ikimuonesha baba na mwana wakiwa na furaha kwelikweli.Baada ya kuposti video hiyo, mashabiki waliibuka na kuanza kumshambulia Zari kuwa watu na baba zao yeye yuko wapi?“Watu na baba zao, wale Wasauzi (Zari na wanaye Tiffah na Nillan) wako wapi, mbona Simba (Mondi) haendi huko?’’ Aliandika shabiki mmoja.

Hata hivyo, baadhi ya maoni hayaandikiki kwa kuwa yanamuondolea Zari utu, lakini wapo walioonesha kumtetea mwanamama huyo kwa kusema Mobeto alifanya makusudi ili kuwaumiza ‘wake wenzake’ ambao wamezaa na Mondi.

“Kuna wanawake wana makusudi jamani, sasa huyu Hamisa (Mobeto) kumposti baba Dyllan mitandaoni ni makusudi tu, maskini Zari, katulia kimya hata hajibu,’’ aliandika mdau mwingine.

Mbali na Zari kushambuliwa kwa posti hizo kiasi cha kuonekana kuwa yale mahaba yake aliyokuja nayo kwa kasi mpaka kufikia kununuliwa gari kwa sasa yameisha, Mobeto ndiyo kwanza anaonekana ameanza vibweka vyake.Zari na Mondi wamejaaliwa watoto wawili ambao ni Tiffa na Nillan, kabla ya kuachana kwao miaka mitatu iliyopita sababu ikiwa ni Mobeto kuchepuka na jamaa huyo kiasi cha kumbebea hadi mimba

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya Arsène Wengers

  Arsène Wenger ni mmoja wa makocha mashuhuri zaidi katika historia ya soka, hasa kwa mchango wake katika klabu ya Arsenal ya Uingereza. Alizaliwa tarehe 22 Oktoba 1949, huko Strasbourg, Ufaransa. Kazi yake ya ukocha ilianza baada ya kupata shahada ya uchumi na kucheza soka kama mchezaji wa kiwango cha chini. Baada ya kustaafu kutoka kucheza, Wenger alianza kazi yake kama kocha kwa mara ya kwanza huko AS Nancy-Lorraine mwaka 1984. Alifanya kazi kwa muda mfupi huko kabla ya kuhamia AS Monaco mwaka 1987. Akiwa Monaco, aliwasaidia kushinda Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mwaka 1988, jambo lililomfanya apate umaarufu kama kocha mwenye uwezo mkubwa wa kukuza vipaji. Hata hivyo, baada ya miaka kadhaa Monaco, Wenger aliachishwa kazi mwaka 1994 kutokana na matokeo mabaya, na akahamia klabu ya Grampus Eight huko Japan mwaka 1995, ambapo alipata mafanikio ya haraka kwa kushinda Kombe la Mfalme. Mwaka 1996, Wenger aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Arsenal, na hapo ndipo alipoanza kuwa maarufu zaid...

UMUHIMU WA KUFANYA SERVICE OIL KWENYE GARI LAKO

  Kufanya **ervice oil* kwenye gari ni muhimu sana kwa utunzaji na ufanisi wa injini. Hapa kuna sababu kuu za kufanya huduma hii mara kwa mara:    1.Kulinda na Kudumisha Injini - Mafuta ya injini husaidia kulainisha sehemu za injini ili zisichakazane haraka kutokana na msuguano.   - Huondoa uchafu na masalia yanayoweza kuzuia utendaji mzuri wa injini.   2. Kuboresha Utendaji wa Gari - Injini inayopata huduma ya mara kwa mara hufanya kazi kwa ufanisi zaidi.   - Inapunguza msuguano wa sehemu za ndani ya injini, hivyo kuongeza nguvu na utendaji wake.   3.Kuongeza Uhai wa Injini - Mafuta machafu yanaweza kusababisha uchakavu wa injini haraka.   - Kubadilisha mafuta mara kwa mara husaidia injini kudumu kwa muda mrefu bila matatizo makubwa.   4.Kupunguza Matumizi ya Mafuta (Fuel Consumption) - Injini safi na yenye mafuta mazuri hufanya kazi vizuri bila kutumia mafuta mengi.   - Mafuta mabovu au machafu y...

KESI INAYO MSUMBUWA MSANII SEAN COMBS MAARU KWA JINA P.DIDDY

 Sean Combs Anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii P. Diddy ni mojawapo ya kesi zinazoibua mjadala mkubwa katika ulimwengu wa burudani na sheria. Katika miaka ya hivi karibuni, P. Diddy amekuwa akihusishwa na mashtaka kadhaa yanayohusiana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia, matumizi mabaya ya madaraka, na unyanyasaji wa kimwili. Moja ya kesi za hivi karibuni ambazo zimechukua nafasi kubwa ni ile inayomuhusisha msanii wa kike aliyewahi kuwa chini ya lebo ya Bad Boy Records, inayomilikiwa na Diddy. Msanii huyo alitoa tuhuma nzito dhidi ya P. Diddy, akidai kuwa alinyanyaswa kingono na kihisia wakati wa uhusiano wao wa kikazi. Msanii huyo anadai kwamba P. Diddy alitumia nguvu na vitisho ili kudhibiti maisha yake binafsi na ya kitaaluma. Kesi hii imevuta hisia na tahadhari kubwa kutoka kwa mashabiki, vyombo vya habari, na wanasheria. Wengi wameibua maswali kuhusu utamaduni wa unyanyasaji na ukatili katika tasnia ya muziki, hasa miongoni mwa watu wenye nguvu kama P. Diddy. Katika ut...