Skip to main content

Ndoa ya Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ Na Zuhura Othuman ‘Zuchu’, October 2

 

LICHA ya mwenyewe kutoanika kinaga ubaga kuhusu mkewe mtarajiwa, lakini kuna mambo yameanikwa ambayo yanashangaza endapo staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ataamua kuingia kwenye ndoa na mtoto mzuri Zuhura Othuman ‘Zuchu’, IJUMAA WIKIENDA linakupa habari mpya inayowahusu!


MNAJIMU AFUNGUKA

Hiyo imetokana na gazeti hili kuzungumza na Mnajimu Maalim Hassan Yahya Hussein, ambaye pamoja na mambo mengine, ameeleza maajabu ya nyota za wawili hao na jinsi ambavyo zinashabihiana na kwamba, watafanya makubwa wakiwa pamoja.


“Zuchu na Mondi nyota zao zinaendana, kwa sababu ni mizani na ng’e, maana ni nyota ambazo ziko jirani, kama wataamua kuwa pamoja na kuoana, watakaa vizuri.


“Katika mwezi wa kumi mwishoni, inaanza nyota ya ng’e, hivyo Diamond kazaliwa Oktoba nyota yake ni mizani na Zuchu kazaliwa Novemba nyota yake ni ng’e, ndivyo nyota zao zinavyoonesha jinsi gani zilivyo karibu.


ATAJA ASILI…

“Mwenye nyota ya ng’e asili yake ni maji na nyota ya mizani asili yake ni hewa, ukiangalia kemistri hapo, maji yanatengenezwa na hewa, hivyo kati yao mmoja anamtengeneza mwingine (Mondi anamtengeneza Zuchu).


“Kile wanachokifanya Zuchu na Diamond, ndicho kinachotakiwa kuwa kama sayansi inavyoonyesha, hiyo ni sawa sawa kabisa hata katika masuala ya kimuziki, ni sawa jinsi Diamond anavyomshika mkono Zuchu kwa sababu ni muingiliano na kuendana kwa nyota zao,’’ alisema Maalim.


DIAMOND KUCHELEWA KUOA

Mbali na kutabiri juu ya ndoa ya Mondi na Zuchu, Maalim aliongeza kwa kusema kuwa, nyota ya Mondi asili yao wana kawaida ya kuchelewa kuoa.


“Watu wenye nyota ya mizani huchelewa kuoa na akiamua kuoa, anaangalia nini atapata kama ni faida ama hasara. “Sababu hiyo huwafanya kuchukua muda mrefu na anakuwa si yeye, bali ni nyota yake inamsukuma kufanya hivyo.


“Kama Diamond kasema anataka kuoa mwaka huu, basi na itakuwa hivyo, kinyota ndivyo inavyoonyesha, pia nyota zao ni za mapenzi na wanapendwa mno,’’ alimalizia kwa kusema Maalim Hassan.


Katika moja ya kauli ambazo Mondi aliwahi kuzungumza kwenye vyombo vya habari ni kuwa, Oktoba 2 mwaka huu ambayo ni siku yake ya kuzaliwa ataoa, lakini hakutaja mhusika atakayefunga naye ndoa hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

RIHANNA APIGA ZENGE MALAWI: MSANII ATOA SOMO KWA DUNIA KUHUSU KUJITOA KATIKA JAMII

📍 Lilongwe, Malawi | 🗓️ Leo Leo historia imeandikwa tena nchini Malawi baada ya msanii maarufu wa kimataifa **Rihanna** kuonyesha mfano wa kipekee wa upendo na kujitoa kwa jamii. Ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kibinadamu kupitia Clara Lionel Foundation, Rihanna hakuja tu kwa ajili ya picha na mahojiano – alifika kazini, akavaa mavazi mepesi, akashika ndoo, na kuungana na wananchi kubeba zenge na kusaidia katika ujenzi wa hospitali ya kijamii. ### 👉 Rihanna Akiwa Mchakamchaka Kazini Mashuhuda wa tukio hilo walisema awali walidhani ni tukio la kawaida la “celebrity visit”, lakini walishangazwa walipoona Rihanna mwenyewe akijitolea kushiriki moja kwa moja katika shughuli za ujenzi. Alionekana akibeba zege, kuchanganya mchanga na simenti, na hata kuwasaidia akina mama waliofika kushiriki kazi hiyo ya kijamii. > “Hatukuwahi kufikiria mtu maarufu kama yeye anaweza kushika koleo na kufanya kazi bega kwa bega na sisi,” alisema mmoja wa wakazi wa kijiji hicho kwa mshangao. ### 🎯 Lengo ...

S2Kizzy: Kutoka Mbeya Mpaka Pluto Republic – Safari ya Mfalme wa Beats za Bongo

  Maisha ya S2Kizzy: Safari ya Mtayarishaji Bora wa Muziki Tanzania Salmin Kasimu Maengo, anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii S2Kizzy au Zombie, alizaliwa tarehe 9 Mei 1996 huko Mbeya, Tanzania. Baada ya mama yake kufariki akiwa na umri wa miaka mitatu, alilelewa na shangazi yake. Baba yake aliondoka na kuoa tena, hali iliyomfanya S2Kizzy kukua katika mazingira ya changamoto. Alianza kujifunza muziki akiwa mdogo, akicheza ngoma shuleni. Wakati wa masomo yake katika shule ya sekondari ya bweni ya Kwiro Boys High School huko Morogoro, alijifunza kutengeneza muziki kwa kutumia kompyuta ya mwalimu wake. Alitumia likizo zake kubaki shuleni, akidai kuwa alikuwa amepewa adhabu, ili aweze kuendelea na mafunzo yake ya muziki. Kipaji na Mafanikio S2Kizzy alijizolea umaarufu mkubwa kwa kutayarisha nyimbo maarufu kama "Tetema" na "Amaboko" za Rayvanny akimshirikisha Diamond Platnumz. Amefanya kazi na wasanii wakubwa kama Diamond Platnumz, Rayvanny, Vanessa Mdee, Bill Nass, ...

Mariah Carey Apata Pigo Kubwa: Mama na Dada Yake Wafariki Katika Siku Moja

 Mariah Carey ni mmoja wa wasanii wenye vipaji vya kipekee na wenye ushawishi mkubwa katika tasnia ya muziki duniani. Amejulikana kwa sauti yake yenye upana wa oktava tano, uwezo wa kutumia miondoko ya melisma, na matumizi ya kipekee ya "whistle register". Katika mwaka wa 2023, aliorodheshwa kama msanii wa tano bora wa wakati wote na jarida la Rolling Stone. citeturn0search12 Maisha ya Awali na Mwanzo wa Muziki Mariah alizaliwa tarehe 27 Machi 1969 huko Huntington, New York. Alikuwa mtoto wa tatu wa Alfred Roy Carey, mhandisi mwenye asili ya Kiafrika na Kivenezuela, na Patricia Hickey, mwalimu wa muziki na mwimbaji wa opera mwenye asili ya Kiayalandi. Baada ya wazazi wake kutalikiana mwaka 1973, Mariah alikulia na mama yake, ambaye aligundua kipaji chake cha muziki akiwa na umri mdogo. Alianza kuandika nyimbo na kufanya maonyesho akiwa shule ya upili, na baada ya kuhitimu, alihamia Manhattan kufuata ndoto yake ya muziki. citeturn0search15 Mafanikio yake yalianza alipo...