Skip to main content

Ndoa ya Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ Na Zuhura Othuman ‘Zuchu’, October 2

 

LICHA ya mwenyewe kutoanika kinaga ubaga kuhusu mkewe mtarajiwa, lakini kuna mambo yameanikwa ambayo yanashangaza endapo staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ataamua kuingia kwenye ndoa na mtoto mzuri Zuhura Othuman ‘Zuchu’, IJUMAA WIKIENDA linakupa habari mpya inayowahusu!


MNAJIMU AFUNGUKA

Hiyo imetokana na gazeti hili kuzungumza na Mnajimu Maalim Hassan Yahya Hussein, ambaye pamoja na mambo mengine, ameeleza maajabu ya nyota za wawili hao na jinsi ambavyo zinashabihiana na kwamba, watafanya makubwa wakiwa pamoja.


“Zuchu na Mondi nyota zao zinaendana, kwa sababu ni mizani na ng’e, maana ni nyota ambazo ziko jirani, kama wataamua kuwa pamoja na kuoana, watakaa vizuri.


“Katika mwezi wa kumi mwishoni, inaanza nyota ya ng’e, hivyo Diamond kazaliwa Oktoba nyota yake ni mizani na Zuchu kazaliwa Novemba nyota yake ni ng’e, ndivyo nyota zao zinavyoonesha jinsi gani zilivyo karibu.


ATAJA ASILI…

“Mwenye nyota ya ng’e asili yake ni maji na nyota ya mizani asili yake ni hewa, ukiangalia kemistri hapo, maji yanatengenezwa na hewa, hivyo kati yao mmoja anamtengeneza mwingine (Mondi anamtengeneza Zuchu).


“Kile wanachokifanya Zuchu na Diamond, ndicho kinachotakiwa kuwa kama sayansi inavyoonyesha, hiyo ni sawa sawa kabisa hata katika masuala ya kimuziki, ni sawa jinsi Diamond anavyomshika mkono Zuchu kwa sababu ni muingiliano na kuendana kwa nyota zao,’’ alisema Maalim.


DIAMOND KUCHELEWA KUOA

Mbali na kutabiri juu ya ndoa ya Mondi na Zuchu, Maalim aliongeza kwa kusema kuwa, nyota ya Mondi asili yao wana kawaida ya kuchelewa kuoa.


“Watu wenye nyota ya mizani huchelewa kuoa na akiamua kuoa, anaangalia nini atapata kama ni faida ama hasara. “Sababu hiyo huwafanya kuchukua muda mrefu na anakuwa si yeye, bali ni nyota yake inamsukuma kufanya hivyo.


“Kama Diamond kasema anataka kuoa mwaka huu, basi na itakuwa hivyo, kinyota ndivyo inavyoonyesha, pia nyota zao ni za mapenzi na wanapendwa mno,’’ alimalizia kwa kusema Maalim Hassan.


Katika moja ya kauli ambazo Mondi aliwahi kuzungumza kwenye vyombo vya habari ni kuwa, Oktoba 2 mwaka huu ambayo ni siku yake ya kuzaliwa ataoa, lakini hakutaja mhusika atakayefunga naye ndoa hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya Arsène Wengers

  Arsène Wenger ni mmoja wa makocha mashuhuri zaidi katika historia ya soka, hasa kwa mchango wake katika klabu ya Arsenal ya Uingereza. Alizaliwa tarehe 22 Oktoba 1949, huko Strasbourg, Ufaransa. Kazi yake ya ukocha ilianza baada ya kupata shahada ya uchumi na kucheza soka kama mchezaji wa kiwango cha chini. Baada ya kustaafu kutoka kucheza, Wenger alianza kazi yake kama kocha kwa mara ya kwanza huko AS Nancy-Lorraine mwaka 1984. Alifanya kazi kwa muda mfupi huko kabla ya kuhamia AS Monaco mwaka 1987. Akiwa Monaco, aliwasaidia kushinda Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mwaka 1988, jambo lililomfanya apate umaarufu kama kocha mwenye uwezo mkubwa wa kukuza vipaji. Hata hivyo, baada ya miaka kadhaa Monaco, Wenger aliachishwa kazi mwaka 1994 kutokana na matokeo mabaya, na akahamia klabu ya Grampus Eight huko Japan mwaka 1995, ambapo alipata mafanikio ya haraka kwa kushinda Kombe la Mfalme. Mwaka 1996, Wenger aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Arsenal, na hapo ndipo alipoanza kuwa maarufu zaid...

UMUHIMU WA KUFANYA SERVICE OIL KWENYE GARI LAKO

  Kufanya **ervice oil* kwenye gari ni muhimu sana kwa utunzaji na ufanisi wa injini. Hapa kuna sababu kuu za kufanya huduma hii mara kwa mara:    1.Kulinda na Kudumisha Injini - Mafuta ya injini husaidia kulainisha sehemu za injini ili zisichakazane haraka kutokana na msuguano.   - Huondoa uchafu na masalia yanayoweza kuzuia utendaji mzuri wa injini.   2. Kuboresha Utendaji wa Gari - Injini inayopata huduma ya mara kwa mara hufanya kazi kwa ufanisi zaidi.   - Inapunguza msuguano wa sehemu za ndani ya injini, hivyo kuongeza nguvu na utendaji wake.   3.Kuongeza Uhai wa Injini - Mafuta machafu yanaweza kusababisha uchakavu wa injini haraka.   - Kubadilisha mafuta mara kwa mara husaidia injini kudumu kwa muda mrefu bila matatizo makubwa.   4.Kupunguza Matumizi ya Mafuta (Fuel Consumption) - Injini safi na yenye mafuta mazuri hufanya kazi vizuri bila kutumia mafuta mengi.   - Mafuta mabovu au machafu y...

KESI INAYO MSUMBUWA MSANII SEAN COMBS MAARU KWA JINA P.DIDDY

 Sean Combs Anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii P. Diddy ni mojawapo ya kesi zinazoibua mjadala mkubwa katika ulimwengu wa burudani na sheria. Katika miaka ya hivi karibuni, P. Diddy amekuwa akihusishwa na mashtaka kadhaa yanayohusiana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia, matumizi mabaya ya madaraka, na unyanyasaji wa kimwili. Moja ya kesi za hivi karibuni ambazo zimechukua nafasi kubwa ni ile inayomuhusisha msanii wa kike aliyewahi kuwa chini ya lebo ya Bad Boy Records, inayomilikiwa na Diddy. Msanii huyo alitoa tuhuma nzito dhidi ya P. Diddy, akidai kuwa alinyanyaswa kingono na kihisia wakati wa uhusiano wao wa kikazi. Msanii huyo anadai kwamba P. Diddy alitumia nguvu na vitisho ili kudhibiti maisha yake binafsi na ya kitaaluma. Kesi hii imevuta hisia na tahadhari kubwa kutoka kwa mashabiki, vyombo vya habari, na wanasheria. Wengi wameibua maswali kuhusu utamaduni wa unyanyasaji na ukatili katika tasnia ya muziki, hasa miongoni mwa watu wenye nguvu kama P. Diddy. Katika ut...