Skip to main content

Serikali imewapongeza wasanii, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali Salehe 'Ali Kiba.


Serikali imewapongeza wasanii, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali Salehe 'Ali Kiba' kwa kuitangaza na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania nje ya nchi.
Hayo yalielezwa jana bungeni na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk.Harisson Mwakyembe wakati akiwasilisha bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2020-2021.
Waziri Mwakyembe alisema kwa kuzingatia ubunifu uliotukuka, wasanii wa Tanzania wameweza kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania nje ikiwa ni pamoja na kuitangaza nchi.
Aliwataja wasanii wengine walioitangaza vyema nchi kuwa ni Rajabu Abdul Kahali ‘Harmonize’, Vanessa Mdee, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, Sharif Thabeet ‘Darassa’, Raymond Mwakyusa ‘Rayvanny’ na wengine wengi.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwapongeza sana wasanii hawa na kuwaasa wengine kuongeza kasi na ubunifu katika kazi zao ili zivutie masoko ya ndani na nje ya nchi,” alisema Mwakyembe.
Aliongeza kuwa Baraza la Sanaa ya Taifa (BASATA) limetoa jumla ya vibali 1,620 kwa wasanii wa Tanzania kwenda nje ya nchi kufanya shughuli za sanaa hadi Machi, 2020.
Pia katika kipindi cha Julai, 2019 hadi Machi, 2020 vibali vilivyotolewa na BASATA kwa muktadha huo ni 135.
Vilevile, Baraza limetoa jumla ya vibali 527 kwa wadau kuingiza wasanii wa nje ya nchi kufanya shughuli za sanaa nchini ili kujifunza sanaa ya Tanzania ambapo vibali 25 vimetolewa katika kipindi cha Julai 2019 hadi Machi, 2020.
Pia Baraza kwa kushirikiana na ubalozi wa India nchini, lilipeleka kikundi cha sanaa cha Lumumba Theatre Group kushiriki katika Tamasha la 34 la Kimataifa la kazi za Sanaa lililofanyika Surajkund nchini India.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya Arsène Wengers

  Arsène Wenger ni mmoja wa makocha mashuhuri zaidi katika historia ya soka, hasa kwa mchango wake katika klabu ya Arsenal ya Uingereza. Alizaliwa tarehe 22 Oktoba 1949, huko Strasbourg, Ufaransa. Kazi yake ya ukocha ilianza baada ya kupata shahada ya uchumi na kucheza soka kama mchezaji wa kiwango cha chini. Baada ya kustaafu kutoka kucheza, Wenger alianza kazi yake kama kocha kwa mara ya kwanza huko AS Nancy-Lorraine mwaka 1984. Alifanya kazi kwa muda mfupi huko kabla ya kuhamia AS Monaco mwaka 1987. Akiwa Monaco, aliwasaidia kushinda Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mwaka 1988, jambo lililomfanya apate umaarufu kama kocha mwenye uwezo mkubwa wa kukuza vipaji. Hata hivyo, baada ya miaka kadhaa Monaco, Wenger aliachishwa kazi mwaka 1994 kutokana na matokeo mabaya, na akahamia klabu ya Grampus Eight huko Japan mwaka 1995, ambapo alipata mafanikio ya haraka kwa kushinda Kombe la Mfalme. Mwaka 1996, Wenger aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Arsenal, na hapo ndipo alipoanza kuwa maarufu zaid...

UMUHIMU WA KUFANYA SERVICE OIL KWENYE GARI LAKO

  Kufanya **ervice oil* kwenye gari ni muhimu sana kwa utunzaji na ufanisi wa injini. Hapa kuna sababu kuu za kufanya huduma hii mara kwa mara:    1.Kulinda na Kudumisha Injini - Mafuta ya injini husaidia kulainisha sehemu za injini ili zisichakazane haraka kutokana na msuguano.   - Huondoa uchafu na masalia yanayoweza kuzuia utendaji mzuri wa injini.   2. Kuboresha Utendaji wa Gari - Injini inayopata huduma ya mara kwa mara hufanya kazi kwa ufanisi zaidi.   - Inapunguza msuguano wa sehemu za ndani ya injini, hivyo kuongeza nguvu na utendaji wake.   3.Kuongeza Uhai wa Injini - Mafuta machafu yanaweza kusababisha uchakavu wa injini haraka.   - Kubadilisha mafuta mara kwa mara husaidia injini kudumu kwa muda mrefu bila matatizo makubwa.   4.Kupunguza Matumizi ya Mafuta (Fuel Consumption) - Injini safi na yenye mafuta mazuri hufanya kazi vizuri bila kutumia mafuta mengi.   - Mafuta mabovu au machafu y...

KESI INAYO MSUMBUWA MSANII SEAN COMBS MAARU KWA JINA P.DIDDY

 Sean Combs Anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii P. Diddy ni mojawapo ya kesi zinazoibua mjadala mkubwa katika ulimwengu wa burudani na sheria. Katika miaka ya hivi karibuni, P. Diddy amekuwa akihusishwa na mashtaka kadhaa yanayohusiana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia, matumizi mabaya ya madaraka, na unyanyasaji wa kimwili. Moja ya kesi za hivi karibuni ambazo zimechukua nafasi kubwa ni ile inayomuhusisha msanii wa kike aliyewahi kuwa chini ya lebo ya Bad Boy Records, inayomilikiwa na Diddy. Msanii huyo alitoa tuhuma nzito dhidi ya P. Diddy, akidai kuwa alinyanyaswa kingono na kihisia wakati wa uhusiano wao wa kikazi. Msanii huyo anadai kwamba P. Diddy alitumia nguvu na vitisho ili kudhibiti maisha yake binafsi na ya kitaaluma. Kesi hii imevuta hisia na tahadhari kubwa kutoka kwa mashabiki, vyombo vya habari, na wanasheria. Wengi wameibua maswali kuhusu utamaduni wa unyanyasaji na ukatili katika tasnia ya muziki, hasa miongoni mwa watu wenye nguvu kama P. Diddy. Katika ut...