Skip to main content
CORONA: MAITI ZA WAAFRIKA ZITATAPAKAA MITAANI – MELINDA GATES
MELINDA GATES, mke wa bilionea Bill Gates wa Marekani, ameonya kwamba iwapo dunia na hususani Afrika haitachukua hatua za haraka za kukabiliana na janga la virusi vya Corona vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19, maiti za Waafrika zitatapakaa katika kila mitaa ya Afrika mijini na Vijijini.
Bi Gates ametoa onyo hilo akizungumza na shirika la habari CNN la Marekani, kuhusu athari kubwa itakayozikumba nchi masikini duniani hususani Afrika.
Alisema moyo wake uko Afrika na kwamba ana wasiwasi mkubwa kwamba bara hilo huenda likashindwa kukabili madhara makubwa ya virusi hivyo.
“Litakuwa janga la kutisha katika nchi zinazoendelea. Baadhi ya sababu zinazoonyesha kwamba idadi haijafikia hali mbaya Afrika, ni kwa kuwa watu wengi hawapimwi kutokana na Afrika kukabiliwa na uhaba wa vifaa vya kupima na hata pale watu wanapopimwa mamlaka za Afrika zimekuwa zikificha baadhi ya taarifa na kuripoti takwimu za visa vya Corona chini ya kiwango. Kinachotokea Ecuador ni kwamba maiti zinatupwa mitaani. Jambo hili litatokea katika nchi za Afrika hivi karibuni,” amesema Melinda Gates.
Melinda ameongeza kuwa kama Afrika itaendelea kutochukua tahadhari zenye tija ni wazi kwamba mwezi May, June na July zitakuwa ni nyakati ngumu na mbaya sana kwa vifo na maambukizi yatokanayo na COVID-19.
"Nafuatilia kila kinachoendelea Afrika, natazama na kusoma kila kinachofanyika Afrika katika kupambana na Corona Virus. Ninasikitika kusema hapa kwamba Afrika bado inafanya mzaha kwenye janga hili" ameongeza Melinda.
Melinda ambaye ni mwenyekiti-mwenza wa taasisi ya Bill and Melinda Gates, ana wasiwasi hali itakuwa mbaya zaidi barani Afrika kutokana na mifumo duni ya tiba na ukosefu wa misaada ya kibinadamu.
Kwa mujibu wake, kitu muhimu alichokishuhudia ni pale China ilipoamua kuwaweka watu wake wengi chini ya karantini.
Aliongeza kwamba amewahi kutembelea miji na vitongoji vingi masikini barani Afrika na sasa anajiuliza ni vipi watu wa bara hilo watalikabili janga hili? Kwani si rahisi kuishi katika mazingira ya usafi na afya katika maeneo hayo.
Melinda ametumia fursa hiyo kuionya Afrika iache kuficha takwimu halisi za visa vya maambukizi ya Corona Virus na vifo. Amesema ni muhimu matukio hayo kutangazwa kama yalivyo ili yawezeshe si tu wananchi wengine kujua hali halisi na hatari ya janga hili ili waongeze tahadhari bali pia amesema uwazi wa hali ya COVID-19 barani Afrika utawezesha Mataifa tajiri na mashirika kufikiri namna ya kuisaidia Afrika.
Aidha Melinda amezitaka Serikali za Afrika kuwekeza zaidi katika kununua vifaa vya kukabiliana na COVID-19 ikiwemo ununuzi wa mashine za oksijen "Ventilators" na vifaa vya maabara ili kuongeza kasi ya upimaji.
NOTE: Onyo hili kutoka kwa Melinda Gates linakuja siku chache tu baada ya maonyo kama hayo kutolewa na Marekani, Shirika la Afya Duniani (WHO) na Bill Gates.
Mimi nadhani badala ya Afrika kuwachukia wanaotuonya ni vema tukafanyia kazi maonyo wanayotupatia.
Nami naamini kuwa Afrika hatupo serious hadi sasa. Mfano wakati tunapiga kelele ili mikusanyiko yote ipigwe marufuku, leo naona tangazo kuwa kumeandaliwa maombi ya kitaifa hapa Tanzania.
Yani tunasema mikusanyiko ipigwe marufuku, lakini serikali inakusanya watu kufanya maombi.
Ni lini Tanzania itafahamu na kukubali kwamba janga la Corona Virus ni tatizo la kisayansi zaidi kuliko kiroho (maombi)? Hebu tujitofautishe kidogo na KINJEKITILE Ngwale. Hizi mbinu za KINJEKITILE katika kukabiliana na Corona Virus itatuletea msiba mkubwa. Afrika iikabili Corona Virus kwa kutumia mbinu za kisayansi.
Ni lini Afrika itaukubali ukweli kuwa Corona haijui mikusanyiko ipi ni ya lazima na ipi siyo ya lazima? Corona haijui tofauti ya mikusanyiko ya maombi, Makanisani, Misikitini, vilabu vya Pombe, minada wala masoko na wala haigopi maeneo hayo.
Afrika ifahamu na kukumbuka kuwa waliotuletea taarifa Kanda Corona Virus ni wanasayansi na wala sio Wachungaji, mitume, manabii na wanasiasa. Afrika ijiulize je ni kwa nini tumewaamini wanasayansi kwamba Corona ipo na inaua haraka sana, lakini hatuwaamini na kufuata mbinu za kujikinga na kuishinda Corona Virus wanazotuelekeza? Sikiliza wataalamu, fanya vile wasemavyo ndiposa uombe Mungu. Kumbuka kuwa hata Mwinjilisti Luka Mtakatifu alikuwa Daktari na alikuwa Mwinjilisti lakini aliwatibu wagonjwa kwa dawa kwanza kabla ya maombi.
Hawa wachungaji feki, manabii na mitume wa UONGO wa leo huo unabii kuwa Corona inaweza kutoweshwa kwa maombi tu wao wameutoa wapi?
Maombi ya siku tatu tumeona matokeo yake, namba inasoma 254, tungoje haya maombi mengine ya kitaifa kama namba haijasoma 500+.
Hatukatai maombi ila sayansi iheshimiwe na ipewe kipaumbele. Serikali ikanunue ventilators za kusaidia upumuaji za kutosha zisambazwe nchi nzima na pia maabara za kupima Corona Virus zisimikwe kila Kanda na kila mkoa.
Pesa zichukuliwe kutoka mfuko wa majanga na kutoka hizi zinazochangishw
a achilia mbali zile za mwenge na Sikukuu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya Arsène Wengers

  Arsène Wenger ni mmoja wa makocha mashuhuri zaidi katika historia ya soka, hasa kwa mchango wake katika klabu ya Arsenal ya Uingereza. Alizaliwa tarehe 22 Oktoba 1949, huko Strasbourg, Ufaransa. Kazi yake ya ukocha ilianza baada ya kupata shahada ya uchumi na kucheza soka kama mchezaji wa kiwango cha chini. Baada ya kustaafu kutoka kucheza, Wenger alianza kazi yake kama kocha kwa mara ya kwanza huko AS Nancy-Lorraine mwaka 1984. Alifanya kazi kwa muda mfupi huko kabla ya kuhamia AS Monaco mwaka 1987. Akiwa Monaco, aliwasaidia kushinda Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mwaka 1988, jambo lililomfanya apate umaarufu kama kocha mwenye uwezo mkubwa wa kukuza vipaji. Hata hivyo, baada ya miaka kadhaa Monaco, Wenger aliachishwa kazi mwaka 1994 kutokana na matokeo mabaya, na akahamia klabu ya Grampus Eight huko Japan mwaka 1995, ambapo alipata mafanikio ya haraka kwa kushinda Kombe la Mfalme. Mwaka 1996, Wenger aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Arsenal, na hapo ndipo alipoanza kuwa maarufu zaid...

UMUHIMU WA KUFANYA SERVICE OIL KWENYE GARI LAKO

  Kufanya **ervice oil* kwenye gari ni muhimu sana kwa utunzaji na ufanisi wa injini. Hapa kuna sababu kuu za kufanya huduma hii mara kwa mara:    1.Kulinda na Kudumisha Injini - Mafuta ya injini husaidia kulainisha sehemu za injini ili zisichakazane haraka kutokana na msuguano.   - Huondoa uchafu na masalia yanayoweza kuzuia utendaji mzuri wa injini.   2. Kuboresha Utendaji wa Gari - Injini inayopata huduma ya mara kwa mara hufanya kazi kwa ufanisi zaidi.   - Inapunguza msuguano wa sehemu za ndani ya injini, hivyo kuongeza nguvu na utendaji wake.   3.Kuongeza Uhai wa Injini - Mafuta machafu yanaweza kusababisha uchakavu wa injini haraka.   - Kubadilisha mafuta mara kwa mara husaidia injini kudumu kwa muda mrefu bila matatizo makubwa.   4.Kupunguza Matumizi ya Mafuta (Fuel Consumption) - Injini safi na yenye mafuta mazuri hufanya kazi vizuri bila kutumia mafuta mengi.   - Mafuta mabovu au machafu y...

KESI INAYO MSUMBUWA MSANII SEAN COMBS MAARU KWA JINA P.DIDDY

 Sean Combs Anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii P. Diddy ni mojawapo ya kesi zinazoibua mjadala mkubwa katika ulimwengu wa burudani na sheria. Katika miaka ya hivi karibuni, P. Diddy amekuwa akihusishwa na mashtaka kadhaa yanayohusiana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia, matumizi mabaya ya madaraka, na unyanyasaji wa kimwili. Moja ya kesi za hivi karibuni ambazo zimechukua nafasi kubwa ni ile inayomuhusisha msanii wa kike aliyewahi kuwa chini ya lebo ya Bad Boy Records, inayomilikiwa na Diddy. Msanii huyo alitoa tuhuma nzito dhidi ya P. Diddy, akidai kuwa alinyanyaswa kingono na kihisia wakati wa uhusiano wao wa kikazi. Msanii huyo anadai kwamba P. Diddy alitumia nguvu na vitisho ili kudhibiti maisha yake binafsi na ya kitaaluma. Kesi hii imevuta hisia na tahadhari kubwa kutoka kwa mashabiki, vyombo vya habari, na wanasheria. Wengi wameibua maswali kuhusu utamaduni wa unyanyasaji na ukatili katika tasnia ya muziki, hasa miongoni mwa watu wenye nguvu kama P. Diddy. Katika ut...