Skip to main content
CORONA: MAITI ZA WAAFRIKA ZITATAPAKAA MITAANI – MELINDA GATES
MELINDA GATES, mke wa bilionea Bill Gates wa Marekani, ameonya kwamba iwapo dunia na hususani Afrika haitachukua hatua za haraka za kukabiliana na janga la virusi vya Corona vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19, maiti za Waafrika zitatapakaa katika kila mitaa ya Afrika mijini na Vijijini.
Bi Gates ametoa onyo hilo akizungumza na shirika la habari CNN la Marekani, kuhusu athari kubwa itakayozikumba nchi masikini duniani hususani Afrika.
Alisema moyo wake uko Afrika na kwamba ana wasiwasi mkubwa kwamba bara hilo huenda likashindwa kukabili madhara makubwa ya virusi hivyo.
“Litakuwa janga la kutisha katika nchi zinazoendelea. Baadhi ya sababu zinazoonyesha kwamba idadi haijafikia hali mbaya Afrika, ni kwa kuwa watu wengi hawapimwi kutokana na Afrika kukabiliwa na uhaba wa vifaa vya kupima na hata pale watu wanapopimwa mamlaka za Afrika zimekuwa zikificha baadhi ya taarifa na kuripoti takwimu za visa vya Corona chini ya kiwango. Kinachotokea Ecuador ni kwamba maiti zinatupwa mitaani. Jambo hili litatokea katika nchi za Afrika hivi karibuni,” amesema Melinda Gates.
Melinda ameongeza kuwa kama Afrika itaendelea kutochukua tahadhari zenye tija ni wazi kwamba mwezi May, June na July zitakuwa ni nyakati ngumu na mbaya sana kwa vifo na maambukizi yatokanayo na COVID-19.
"Nafuatilia kila kinachoendelea Afrika, natazama na kusoma kila kinachofanyika Afrika katika kupambana na Corona Virus. Ninasikitika kusema hapa kwamba Afrika bado inafanya mzaha kwenye janga hili" ameongeza Melinda.
Melinda ambaye ni mwenyekiti-mwenza wa taasisi ya Bill and Melinda Gates, ana wasiwasi hali itakuwa mbaya zaidi barani Afrika kutokana na mifumo duni ya tiba na ukosefu wa misaada ya kibinadamu.
Kwa mujibu wake, kitu muhimu alichokishuhudia ni pale China ilipoamua kuwaweka watu wake wengi chini ya karantini.
Aliongeza kwamba amewahi kutembelea miji na vitongoji vingi masikini barani Afrika na sasa anajiuliza ni vipi watu wa bara hilo watalikabili janga hili? Kwani si rahisi kuishi katika mazingira ya usafi na afya katika maeneo hayo.
Melinda ametumia fursa hiyo kuionya Afrika iache kuficha takwimu halisi za visa vya maambukizi ya Corona Virus na vifo. Amesema ni muhimu matukio hayo kutangazwa kama yalivyo ili yawezeshe si tu wananchi wengine kujua hali halisi na hatari ya janga hili ili waongeze tahadhari bali pia amesema uwazi wa hali ya COVID-19 barani Afrika utawezesha Mataifa tajiri na mashirika kufikiri namna ya kuisaidia Afrika.
Aidha Melinda amezitaka Serikali za Afrika kuwekeza zaidi katika kununua vifaa vya kukabiliana na COVID-19 ikiwemo ununuzi wa mashine za oksijen "Ventilators" na vifaa vya maabara ili kuongeza kasi ya upimaji.
NOTE: Onyo hili kutoka kwa Melinda Gates linakuja siku chache tu baada ya maonyo kama hayo kutolewa na Marekani, Shirika la Afya Duniani (WHO) na Bill Gates.
Mimi nadhani badala ya Afrika kuwachukia wanaotuonya ni vema tukafanyia kazi maonyo wanayotupatia.
Nami naamini kuwa Afrika hatupo serious hadi sasa. Mfano wakati tunapiga kelele ili mikusanyiko yote ipigwe marufuku, leo naona tangazo kuwa kumeandaliwa maombi ya kitaifa hapa Tanzania.
Yani tunasema mikusanyiko ipigwe marufuku, lakini serikali inakusanya watu kufanya maombi.
Ni lini Tanzania itafahamu na kukubali kwamba janga la Corona Virus ni tatizo la kisayansi zaidi kuliko kiroho (maombi)? Hebu tujitofautishe kidogo na KINJEKITILE Ngwale. Hizi mbinu za KINJEKITILE katika kukabiliana na Corona Virus itatuletea msiba mkubwa. Afrika iikabili Corona Virus kwa kutumia mbinu za kisayansi.
Ni lini Afrika itaukubali ukweli kuwa Corona haijui mikusanyiko ipi ni ya lazima na ipi siyo ya lazima? Corona haijui tofauti ya mikusanyiko ya maombi, Makanisani, Misikitini, vilabu vya Pombe, minada wala masoko na wala haigopi maeneo hayo.
Afrika ifahamu na kukumbuka kuwa waliotuletea taarifa Kanda Corona Virus ni wanasayansi na wala sio Wachungaji, mitume, manabii na wanasiasa. Afrika ijiulize je ni kwa nini tumewaamini wanasayansi kwamba Corona ipo na inaua haraka sana, lakini hatuwaamini na kufuata mbinu za kujikinga na kuishinda Corona Virus wanazotuelekeza? Sikiliza wataalamu, fanya vile wasemavyo ndiposa uombe Mungu. Kumbuka kuwa hata Mwinjilisti Luka Mtakatifu alikuwa Daktari na alikuwa Mwinjilisti lakini aliwatibu wagonjwa kwa dawa kwanza kabla ya maombi.
Hawa wachungaji feki, manabii na mitume wa UONGO wa leo huo unabii kuwa Corona inaweza kutoweshwa kwa maombi tu wao wameutoa wapi?
Maombi ya siku tatu tumeona matokeo yake, namba inasoma 254, tungoje haya maombi mengine ya kitaifa kama namba haijasoma 500+.
Hatukatai maombi ila sayansi iheshimiwe na ipewe kipaumbele. Serikali ikanunue ventilators za kusaidia upumuaji za kutosha zisambazwe nchi nzima na pia maabara za kupima Corona Virus zisimikwe kila Kanda na kila mkoa.
Pesa zichukuliwe kutoka mfuko wa majanga na kutoka hizi zinazochangishw
a achilia mbali zile za mwenge na Sikukuu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Comments

Popular posts from this blog

S2Kizzy: Kutoka Mbeya Mpaka Pluto Republic – Safari ya Mfalme wa Beats za Bongo

  Maisha ya S2Kizzy: Safari ya Mtayarishaji Bora wa Muziki Tanzania Salmin Kasimu Maengo, anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii S2Kizzy au Zombie, alizaliwa tarehe 9 Mei 1996 huko Mbeya, Tanzania. Baada ya mama yake kufariki akiwa na umri wa miaka mitatu, alilelewa na shangazi yake. Baba yake aliondoka na kuoa tena, hali iliyomfanya S2Kizzy kukua katika mazingira ya changamoto. Alianza kujifunza muziki akiwa mdogo, akicheza ngoma shuleni. Wakati wa masomo yake katika shule ya sekondari ya bweni ya Kwiro Boys High School huko Morogoro, alijifunza kutengeneza muziki kwa kutumia kompyuta ya mwalimu wake. Alitumia likizo zake kubaki shuleni, akidai kuwa alikuwa amepewa adhabu, ili aweze kuendelea na mafunzo yake ya muziki. Kipaji na Mafanikio S2Kizzy alijizolea umaarufu mkubwa kwa kutayarisha nyimbo maarufu kama "Tetema" na "Amaboko" za Rayvanny akimshirikisha Diamond Platnumz. Amefanya kazi na wasanii wakubwa kama Diamond Platnumz, Rayvanny, Vanessa Mdee, Bill Nass, ...

RIHANNA APIGA ZENGE MALAWI: MSANII ATOA SOMO KWA DUNIA KUHUSU KUJITOA KATIKA JAMII

📍 Lilongwe, Malawi | 🗓️ Leo Leo historia imeandikwa tena nchini Malawi baada ya msanii maarufu wa kimataifa **Rihanna** kuonyesha mfano wa kipekee wa upendo na kujitoa kwa jamii. Ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kibinadamu kupitia Clara Lionel Foundation, Rihanna hakuja tu kwa ajili ya picha na mahojiano – alifika kazini, akavaa mavazi mepesi, akashika ndoo, na kuungana na wananchi kubeba zenge na kusaidia katika ujenzi wa hospitali ya kijamii. ### 👉 Rihanna Akiwa Mchakamchaka Kazini Mashuhuda wa tukio hilo walisema awali walidhani ni tukio la kawaida la “celebrity visit”, lakini walishangazwa walipoona Rihanna mwenyewe akijitolea kushiriki moja kwa moja katika shughuli za ujenzi. Alionekana akibeba zege, kuchanganya mchanga na simenti, na hata kuwasaidia akina mama waliofika kushiriki kazi hiyo ya kijamii. > “Hatukuwahi kufikiria mtu maarufu kama yeye anaweza kushika koleo na kufanya kazi bega kwa bega na sisi,” alisema mmoja wa wakazi wa kijiji hicho kwa mshangao. ### 🎯 Lengo ...

Rihanna Atangaza Ujauzito wa Tatu kwa Mbwembwe Kwenye Met Gala 2025

 Usiku wa Kipekee wa Rihanna kwenye Met Gala 2025 Usiku wa Mei 5, 2025, Rihanna alifanya tukio lisilosahaulika katika Met Gala kwa kutangaza ujauzito wake wa tatu kwa njia ya kipekee na ya kuvutia. Akiwa amechelewa kama kawaida yake, alifika kwenye Jumba la Makumbusho la Sanaa la Metropolitan akiwa amevalia vazi la Marc Jacobs lililojumuisha koti fupi la pamba nyeusi, korse, na sketi yenye mistari myembamba, pamoja na kofia pana iliyotengenezwa kwa ushirikiano na Stephen Jones. Muonekano huu uliendana na kaulimbiu ya mwaka huu ya “Superfine: Tailoring Black Style,” ambayo iliheshimu mitindo ya mavazi ya Watu Weusi. Rihanna alionyesha tumbo lake la ujauzito kwa kuushika kwa upole mbele ya kamera, bila kutoa tamko lolote rasmi, lakini ishara hiyo ilitosha kuthibitisha habari hiyo. Mpenzi wake, A\$AP Rocky, ambaye alikuwa mwenyeji mwenza wa hafla hiyo, alifika mapema na hakutoa maoni yoyote kuhusu ujauzito huo. Katika mahojiano ya moja kwa moja na NBC News, Shakira alionyesha msisimko...